Karibuni katika blog ya jukwaa la vijana ambayo itakuwa inawaletea habari na taarifa mbalimbali kuhusu maendeleo ya vijana nchini. Blog ya jukwaa la vijana itakupa fursa ya kufahamu nini kimejiri katika vikao vya majukwaa ya vijana ambayo yanaendeshwa katika wilaya 4 za Arusha mjini, Kiteto, Ngorongoro na Kinondoni. Jukwaa la vijana Zanzibar tayari limeshazinduliwa mnamo tarehe 17/01/2009. Juhudi zinafanywa ili kuhakikisha vijana wengi zaidi wanashiriki katika wilaya 5 zaidi mwaka 2009 zikiwemo Pwani, Mtwara mjini, Lindi mjini, Masasi na Ruangwa.
Karibuni kwa maoni na maboresho... Vijana tunaweza tukiwezeshwa na kujiwezesha!