Monday, May 18, 2009

..........Jukwaa la Vijana Zanzibar................

Vijana kutoka Tanzania Zanzibar walipata nafasi ya kukutana na kujadili mambo yanayowahusu vijana wa kutoka kisiwani humo na kutoa kero pamoja na mapendekezo kulingana na kero hizo husika kama ifuatavyo:
KERO:
  1. Ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika vikao vya serikali za mitaa.
  2. Vijana kukosa elimu ya ujasiriamali.
  3. Kutokuaminiwa kwa vijana katika kupewa mikopo.
  4. Vijana kukosa mazingira mazuri ya kufanyia na kuanzisha shughuli za kibiashara.
Na kupendekeza kwamba:
  1. Elimu ya ujuzi na ufundi ianze toka shule ya msingi.
  2. Vijana kupewa kipaumbele katika vyombo vya maamuzi kuanzia ngazi ya chini.
  3. Vijana kupatiwa mwakilishi katika baraza la wawakilishi.
  4. Vijana kupatiwa fursa mbalimbali za kijamii.

No comments: