Tuesday, February 17, 2009

Who are you? A winner or a looser............

Differences between winners and losers written by Munnel James and Dorothy Jongeward.

Winner do.........

-Knows for everything there is a season and for every activity a time
-Have time to be aggressive and a time to be passive.
-have time to be together and a time to be alone.
-Have time to fight and a time to love.
-Have time to cry and a time to laugh.
-Have time to comfort and a time to withdraw.
-Have time to speak and time to silent.
-Have time to hurry and a time to wait.
-To winner time is precious. They don't kill it but live it here and now....

While.............

Losers do....
-Speak of themselves as successful but anxious unsuccessful but trapped or successful but unhappy.
-Occupying their minds with material that that are irrelevant to the current situation.
-Invest their time in maintaining masks, often projecting a phony front.
-Destroying the present by focusing on past memories or future expectations.
-Self-pitying and shifts the responsibility for unsatisfactory life onto others.
-Unable to bring the full potential of their senses into the immediate situation, loser's perceptions are incorrect or incomplete.
"Now we all know were we stand, and so it is our duty to change if we see that our behaviors turns to us to a looser situation, or should improve if we see that what we do is on the winning side so as not to fall on the loosing side later on."
Thank you!

Friday, February 6, 2009

Hongera Kwa Kufanyika Jukwaa Zanzibar......!!!

Baada ya kutoka Arusha mjini, Kiteto na Loliondo Jukwaa lilihamia Zanzibar na ratiba ya Jukwaa ilitoka na kujadiliwa katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa, VUGA Zanzibar siku ya Jumamosi Tarehe 07 na 08 Februari 2009.

Mada zilizojadiliwa katika Jukwaa la Zanzibar lililofanyika Tarehe 07 na 08 Februari 2009.
Jumamosi (07 Februari 2009)
  1. Mfumo wa serikali za Mitaa, Zanzibar (Nafasi ya kijana katika vikao vya utoaji maamuzi)
  2. Nafasi ya kijana katika MKUZA.
Jumapili (08 Februari 2009)
  1. Sera ya Vijana, Zanzibar.

Jukwaa hilo lililofanyika likiwa na lengo la kujenga mahusiano na ushirikiano bora baina ya jumuiya za vijana Tanzania pamoja na serikali kwa lengo la kuondoa matatizo yanayomkabili kijana ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi wa nchi na kupunguza umasikini liliweza kukutanisha vijana themanini na tisa(89) kutoka kwenye mashirika mbali mbali. Ripoti ya jukwaa imetoka na itakuwa katika blog yako muda si mrefu ili na wewe uweze kutoa maoni yako.

Monday, February 2, 2009

Jukwaa la Loliondo 25-26/11/2008

Warsha ya utawala bora na ushirikishaji wa uma katika kufanya maamuzi loliondo 25-26/2008

TYC ilifanya warsha ya utawala bora katika kijiji cha loliondo katika kitongoji cha wasso tarehe 25-26/11/2008,warsha hiyo ilihudhuriwa na vijana wapatao 100 kutoka pande mbalimbali za loliondo ikisimamiwa kwa ukaribu kabisa na ngorongoro Network (NGONET)ambayo ni asasi shiriki ya TYC loliondo

Mkutano ulichukua siku mbili ambapo siku ya kwanza mwezeshaji alipata wasaa wa kutembelea vikundi na kuweza kushawishi kikundi kimoja kujiunga na TYC. Siku ya pili kulikuwa na warsha ambayo ilikuwa inazungumzia mambo ya Utawala Bora.

Utawala Bora
Utawala bora huanza katika ngazi ya chini kabisa na kutanuka hadi ngazi ya juu au kubwa kama ifuatavyo.Binafsi,familia /kaya kitongoji/jamii, kata,tarafa,wilaya,mkoa,kanda,taifa,kimataifa

Vigezo vya Utawala Bora
Uwazi,demokrasia,uadilifu,ukweli usawa,ushirikishwaji,uaminifu,uzalendo mawasiliano,msimamo haki

Baada ya kujadili kwa kupitia njia mbalimbali za kuwezesha uwepo wa utawala bora washiriki walipendekeza kwamba TYC(Asasi iliyoanda warsha) na NGONET(Asasi shiriki) waongeze warsha katika nyanja mbalimbali ili kuwakomboa vijana ili kuwajengea ufahamu.